Jumatano, 6 Aprili 2016

Timu ya Soka ya Tanzania yaigaragaza Marekani.

6 Aprili 2014 - Timu ya Soka ya Mtoto wa Mtaani kutoka Tanzania yashinda Kombe la Dunia. Timu hiyo inayoundwa na watoto kutoka kituo cha Tanzania Street Children Sports Academy (TSCSA) kilichopo jijini Mwanza, Tanzania iliicharaza Burundi magoli 3-1 katika mchezo wa fainali. Mchezaji Frank William alitia kimiani magoli yote matatu yaliyoipa ushindi timu yao kutoka Tanzania. Awali katika hatua ya nusu fainali, Tanzania iliigaragaza vibaya Marekani kwa magoli 6-1. Fainali hizo zilifanyika jijini Rio de Janeiro nchini Brazil. Kombe la Dunia la Mtoto wa Mtaani (Street Child World Cup) huwakutanisha watoto wa mitaani kote duniani.Kuelekea michuano ya mwaka 2014, mwanasoka wa zamani wa Uingereza David Beckham alinukuliwa akisema: “I look forward to Brazil in 2014 when street children from around the world will play football and represent the millions of children who still live or work on our streets.“

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni