Jumatano, 11 Mei 2016

Je, Wajua? Zanzibar iliwahi kuingia katika Kitabu cha Kumbukumbu za Guinness Duniani.

Mnamo tarehe 17 Januari 1961 Uchaguzi wa Baraza la Kutunga Sheria ulifanyika Zanzibar. Afro-Shirazi Party (ASP) ilishinda viti 10, Zanzibar Nationalist Party (ZNP) viti 9 na Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP) viti 3. Zaidi ni kuwa katika jimbo la Chake-Chake ASP ilipata kura 1,538 na ZNP kura 1,537. Hii ni tofauti ya kura moja tu. Katika taarifa ya mwaka ya Kitabu cha Kumbukumbu za Guinness Duniani (Guinness Book of World Records), matokeo haya yalitajwa kama "matokeo yaliyokaribiana sana."

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni