Jumatano, 18 Mei 2016

JE, WAJUA? Mlima Kilimanjaro ulikuwa mlima mrefu kuliko yote katika Dola ya Ujerumani (German Empire).

Mlima Kilimanjaro ulikuwa mlima mrefu kuliko yote katika Dola ya Ujerumani (German Empire) hadi mwaka 1918. Dola ya Ujerumani ilijumuisha Ujerumani yenyewe na makoloni yake yote. Baada ya makoloni yake kujinyakulia uhuru, mlima mrefu zaidi uliobaki Ujerumani ya leo ni Mlima Zugspitze wenye urefu wa mita 2,962. Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu kuliko yote Afrika una urefu wa mita 5,888 kwa mujibu wa vipimo vilivyofanyika mwaka 2014. Tarehe 5 Oktoba 1889 Mtanzania YOHANA LAUWO akiongozana na Mjerumani HANS MEYER na Muaustria LUDWIG PURTSCHELLER wanakuwa watu wa kwanza kufika kilele cha Kilimanjaro.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni